Thursday, August 10, 2017

MSHIKO NJE NJE

Tags

Helping hands international (H2i) ni asasi isiyo ya kiserikali (NGO) ya kimataifa inayojihusisha na kusaidia watu wanyonge na wahitaji wengine.(Yatima,wajane, walemavu,waathirika wa madawa ya kulevya,machangudoa,nk)

Mbeba maono wa H2i ni mama Luzviminda Mac Elvis, kutoka Ufilipino ambaye naye baada ya kupitia maisha magumu sana mwanzoni kutokana na kuzaliwa katika familia duni sana kiasi cha kujikuta anasomeshwa na mtu ambaye hata hakumfahamu kabisa,jambo lililomfanya aamini kuwa licha ya matatizo anayoweza kukutana nayo binadamu yeyote akipata mkono wa msaada anaweza kutimiza ndoto zake. Imani hii ilimfanya atafakari sana juu ya watu wenye matatizo kama aliyoyapitia yeye na ikampelekea sasa kuanzisha Mpango wa kuwasaidia baada ya yeye kuwa amefanikiwa kutokana na kusaidiwa. Akiwa amehitimu masomo yake na kuajiriwa huku akikeleketwa na maono yake ya muda mrefu aliamua kurejea kwao Ufilipino na kuasisi asasi aliyoiita HELPING HANDS.

Pamoja na mambo mengine asasi hii ilijihusisha na kuwasaidia watoto wa mitaani kurejea shule,watoto yatima kuwasomesha, kuwasaidia waathirika wa madawa na machangudoa kurejea hali zao za awali na kuwasaidia kuanzisha miradi itakayowafanya wajitegemee na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Kufanikisha yote haya alikuwa anafadhiriwa na kampuni ya Magari ya Hyundai.

Akiwa anaendelea na kazi zake alikutana na daktari Ramiel Policarpio,ambaye alikuwa ni daktari bingwa wa meno huko nchini Ufilipino. Naye alikuwa na maono yanayokaribiana sana na ya mama Luzviminda. Dr Ramiel alikuwa inajihusisha na kusaidia wajane,wazee na wasiojiweza katika nchi hiyo. Walipokutana wakabaini kuwa maono yao yanafanana na kwamba kwa pamoja wanaguswa na makundi yenye mahitaji maalumu. Waliamua kuunganisha nguvu na kueneza huduma zao nje ya Ufilipino. Kwa hapa na jina la asasi hii likabadilika na kuwa _Helping Hands International_ badala ya *Helping Hands* kama ilivyo kuwa awali. Wakaanza kuenea barani Asia kwa kasi sana kutokana na mguso wa huduma zao kwa jamii. Jambo hili liliwafanya wapatwe na changamoto za kifedha ili kuwasaidia watu wengi waliojitokeza kutokana na udhamini wa awali kuzidiwa kabisa.

Waliamua kutafuta suluhu kwa changamoto hii na waliamua kubuni vyanzo vya mapato ili kuinua na kuendeleza huduma hizi.

Kwanza waliomba udhamini kutoka kampuni kadhaa kubwa duniani, na kutokana na ubayana wa maono yao walipata udhamini kutoka kampuni za Apple,HP,Hyundai, Diamond Bank,GAC Motors, Glo nk(hadi Leo). Asasi pia hupata misaada kutoka kwa watu maarufu wanaotaka kusaidia watu(philanthropist) na asasi mbalimbali kama vile Bill Gates Foundation.

Pili ,waliamua kubuni chanzo kingine cha kipato kutokana na michango ya wanachama ambao nao kwa hiari yao na kuguswa na matatizo ya wanyonge na kuamua kuwa sehemu ya utilikaji wa maono haya watakaojiunga na H2i. Hapa wakaweka mchango unaofanana kwa wanachama wote dunia nzima USD 40 kwa kila mwanachama. Mchango huu unatolewa Mara moja tu kwa maisha yote ya mwanachama.

Ili kuhakikisha wanasambaa zaidi duniani na kuwafikia watu wengi zaidi walibuni mfumo wa biashara unaoweza kufanywa na wanachama wenyewe ili kuwawezesha kujiimarisha kiuchumi kuenea zaidi. Ikaingizwa dhana ya biashara ya Mtandao ya kuwafikia wanachama wapya.

Iko hivi mwanachama anapoelewa maono haya na akaona anaweza kuwa sehemu ya ukamilikaji wake atajiunga na H2i na atasajiriwa kama mwanachama na balozi wa kudumu ( maisha yake yote)na baada ya kusajiriwa naye atawashirikisha wengtano habari hizi ili nao wajiunge chini yake. Mtu mmoja ukimuunganisha utalipwa dola 8(17,600) na kwa kawaida unapaswa angalau uingize watu wawili ambao nao watafanya hivyo kila mmoja. Hauzuiwi kuingiza idadi yoyote ya watu uliyonayo hata kama ni watu 100! japo kiwango cha chini sana ni watu wawili.

Kukawekwa ngazi zitakazotumika kupima utendaji kazi wa mwanachama. Kuna ngazi tano(tutaziangalia baadaye)
ambazo zilipewa vigezo na zawadi zake mbalimbali.

Mfumo huu wa biashara ukaonekana ni bora sana na rahisi kufanya. Asasi hii ilianza kuenea kwa kasi katika mabara mengine nje na Asia na mnamo mwaka 2013 H2i iliingia Afrika kupitia daktari mmoja aitwaye Timothy Odeghe (Nigeria) ambaye alikutana na Dr. Ramiel ( mmoja wa waanzilishi) na Dr Timothy alipowashirikisha juu ya hali duni walizonazo watu wake,waanzilishi walimshirikisha katika maono hayo na akapendezwa nayo na kujiunga. Alipolifikisha wazo hilo lilipokelewa kwa haraka sana na kukua kwa kasi nchini na nje ya nchi pia. Watu wengi wamewezeshwa kufikia ndoto zao na wanaendele .

whatsap 0782 065401

JINSI YA KUTENGENEZA ICE CREAM/LAMBALAMBA NJOO WHATSAP 0782 065401

JINSI  YA  KUTENGENEZA   ICE CREAM/LAMBALAMBA NJOO WHATSAP 0782 065401